Baada ya kuangalia jinsi uchungu unavyoanza hadi kukua, sasa tuone jinsi gani unaweza kuushinda uchungu kabla haujaharibu maisha yako na mahusiano yako.
Kabla hujajaribu kuung’oa uchungu inabidi ujue ni jinsi gani mizizi yake imejikita ardhini. Mizizi ya uchungu inakuwa kutoka kwenye mbegu ambayo ndiyo kosa ulilotendewa. Kosa linaweza kuwa ni tukio fulani au neno au maoni fulani au lugha ya mwili ambalo inawezekana haikukusudiwa / ilikusudiwa kukuudhi na wewe ukaona kuwa huwezi kusamehe. Usipogundua mbegu husika huwezi kung’oa mizizi yake, unaweza kata matawi na shina ila yataendelea kuchipuka hasi utakapoitambua mbegu (chanzo cha uchungu /kutokusamehe) na kung’oa mizizi yake (kusamehe).
Nguvu ya mizizi hutegemea ni kwa kiasi gani uchungu umepaliliwa na kutunzwa. Lazima mawazo yote mabaya yanayoambatana na kutokusamehe yatoke ndipo utakapoweza kuisikia sauti ya Mungu ndani ya dhamira yako inayokutaka kutubu na kuachilia. La sivyo utazidi kujiona upo sahihi na uchungu utazidi kukomaa. Lazima uachane na mawazo yanayokuonyesha wewe uko sawa na mwingine ndio mwenye makosa. Neno la Mungu lazima liingie ndani yako ili uweze kuona jinsi ambavyo Yesu anachukizwa na uchanofanya.
1) Yesu amesema tunapaswa kusamehe mara zote Mathayo 18:21-22
Usitafute sababu ya kutokusamehe, hata kama amekukosea mara nyingi Yesu ameagiza tusamehe saba mara sabini. Jifunze kuwa na msamaha wa kweli, msamaha haumaanishi kiwa hukukosewa bali unapaswa kusamehe kama ambavyo Mungu amekusamehe. Msamaha unasababisha neema ya Mungu kukaa kwa wingi ndani yako. Mume na mke lazima wasameheane katika kila hali, lisiwepo jambi ambalo mtu ataacha kumsamehe mwenzi wake. Muombe Mungu akuwezeshe kuwa na msamaha kila wakati.
2) Kisasi ni cha Mungu tu! Warumi 12:19
Kamwe usilipize kisasi. Unapojaribu kujitafutia haki kwa kulipiza kisasi unajitenga na neema ya Mungu, wewe usilipize ovu kwa ovu bali tenda mema kwa upendo. Warumi 12: 17 biblia inasema tuushinde ubaya kwa wema. Hakikisha unafanya hivyo kwa upendo ili uweze kuwaonyesha neema ya Mungu waliokukosea nao wapate nafasi ya kumrudia Mungu. Jivike upendo, utuwema, fadhili, na samehe hata kama kuna sababu ya kulaumu. Wakolosai 3: 12-13. Kamwe usiweke chuki ndani yako Wakolosai 3:8, onyesha kuwa Yesu anafanya kazi ndani yako kwa kuwa mtu wa msamaha. Kila asubuhi muombe Mungu akujalie neema yake ili uewze kuionyesha kwa watu wote utakaokutana nao kwa siku hiyo.
3) Muamini Mungu katika wakati unapoonewa Mathayo 5:10-12
Maranyingine tunajaribiwa pale ambapo watu wanatutendea visivyo. Yesu anatuamuru tupendane bila kuwa na kinyongo. Biblia inasema kuwa furahi ukiwa katika hali kama hiyo, tumia hiyo nafasi kuushinda ubaya kwa kuwaonyesha upendo. Unaweza tumia nafasi hiyo kuonyesha nguvu ya Mungu, badaya ya kuwa na uchungu samehe na pokea neema ya Mungu ya kukuwezesha kumpenda huyo aliyekukosea. Warumi 12:20-21
Mambo matatu ya kuzingatia
a) Samehe kwa moyo wako wote
b) Mtendee kwa wema na upendo ambao haustahili aliye kukosea
c) Furahi unapoonyesha upendo wa kweli kwa mtu huyo. Kwa kufanya hivyo hakika atauona upendo wa Mungu kupitia kwako.
Ubarikiwe na Bwana. Tutakuja kuangalia sasa hatua za kuondoa uchungu na kinyongo.