Wafilipi – 2: Ukarimu

Matendo 16:13-15
Kutokana na kutokuwa na nyumba ya ibada katika Filipi, Paulo na wenzake walienda kusali kando ya mto na kuwahubiria wanawake waliokuwepo mahali pale. Mmoja wao aitwaye Lidia alipokea neno la Mungu na kuamua kubatizwa, kisha akawakaribisha nyumbani kwake. Baada ya hapo waumini wakawa wanakutanikia hapo.

Matendo 16:40 Nao wakatoka gerezani wakaingia nyumbani mwa Lidia; na walipokwisha kuonana na ndugu wakawafariji, wakaenda. zao.

Kanisa la Filipi lilianzishwa na Paulo kwa msaada wa ukarimu kutoka kwa Lidia aliyetoa nyumba yake iwe mahali pa kukutanikia. Ukarimu huu uliendelea na uliambukizwa kwa kanisa zima na waliendelea kumhudumia Paulo hata alipokuwa mbali nao.

2Korinto 11:9a Nami nilipokuwa pamoja nanyi na kuhitaji sikumlemea mtu. Maana hao ndugu waliokuja kutoka Makedonia walinipa kadiri ya mahitaji yangu.

Filipi 4:18 Lakini ninavyo vitu vyote na kuzidi, tena nimejaa tele; nimepokea kwa mkono wa Epafradito vitu vyote vilivyotoka kwenu, harufu ya manukato, sadaka yenye kibali, impendezayo Mungu.

Filipi 4:16 Kwa kuwa hata huko Thesalonike mliniletea msaada kwa mahitaji yangu, wala si mara moja.

Ukarimu huwa unaendelea na kuzaa ukarimu, ukarimu pia husimamisha huduma na huleta umoja. Tujifunze kuwa wakarimu kwa watumishi wa Mungu kama Lidia na kanisa la Filipi.

Leave a comment