Wakati unapokuwa katika hali nzuri, mambo yako yanaenda kama ulivyopanga, kila kitu kwenye maisha yako kipo kwenye mstari, upo kwenye kilele cha furaha na mafanikio ni rahisi sana kuwatia moyo wengine, kukiri ukuu wa Mungu, kuongea maneno ya kuinua na kuamini kuwa Mungu atakuinua zaidi na zaidi. Ahadi za Mungu unaziona ni zako.
Lakini pale unapokuwa chini, kila unaloshika linafeli, mambo yako yote hayana muelekeo, kila upande ni madeni, magonjwa, shida na matatizo… Inakuwa Mungu sana kuliamini neno la Mungu. Ahadi za Mungu unaziona kama wewe zimekuruka. Unaona kama vile Mungu hayupo, amekuacha na hata mtu akikutia moyo unaona anaongea tu na yale uliyokuwa unayakiri mwanzo sasa unaona kama haiwezekani.
Nakutia moyo mpendwa, haijalishi hali gani unayopitia, Mungu bado ni mwaminifu na ni yeye yule hajabadilika kamwe. Mungu wa wakati wa raha bado ni Mungu hata wakati wa shida, Mungu aliyekufanikisha bado ni Mungu hata ukipita katika magumu, Mungu aliyewavusha wana wa Israel bahari ya shamu bado alikuwa Mungu wakati wa vita. Hakika hatakuacha wala kukupungukia. Usiache kumuamini nyakati zote.