Zaburi 43: 1-4
1 Ee Bwana, unihukumu, unitetee kwa taifa lisilo haki, Uniokoe na mtu wa hila asiye haki.
2 Kwa kuwa Wewe ndiye Mungu uliye nguvu zangu; kwa nini umenitupa? Kwa nini ninakwenda nikihuzunika, adui wakinionea?
3 Niletewe nuru yako na kweli yako ziniongoze, Zinifikishe kwenye mlima wako mtakatifu na hata maskani yako.
4 Hivyo nitakwenda madhabahuni kwa Mungu, kwa Mungu aliye furaha yangu na shangwe yangu;
Nitakusifu kwa kinubi, Ee MUNGU, Mungu wangu.
Nafsi yangu kwa nini kuinama, Na kufadhaika ndani yangu?
Umtumaini Mungu;
Kwa maana nitakuja kumsifu, Aliye afya ya uso wangu,
Na Mungu wangu.